Mwenyezi Mungu ametupa sote akili na uwezo wa kutuwezesha kufanya maamuzi sahihi na ya maana. Nayo ni maamuzi muhimu sana katika maisha ya mwanadamu. Mustakabali wake unautegemea uamuzi huo, kufuatana na hilo, kila mmoja wetu lazima achunguze ushahidi uliotolewa bila kupendelea ndipo achague kile kinachoonekana kuwa ni sahihi mpaka pale ushahidi mwingine utakapotokea.