Hakika kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu, tunamhimidi yeye na tunamtaka msaada yeye, na tunamuomba msamaha, na tunajilinda kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shari ya nafsi zetu, na ubaya wa matendo yetu, aliyemuongoza Mwenyezi Mungu hakuna wa kumpoteza, na aliyempoteza hakuna wa kumuongoa, na ninashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, yeye pekee asiye na mshirika wake, na ninashuhudia kuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake, Amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake, na juu ya watu wake, na maswahaba zake, na ampe amani na salamu nyingi.