Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyoteNa mwisho mwema ni kwa wenye kumcha AllahSala na amani ziwe juu ya mja wake na mtume wake Mtume wetu Muhammad alietumwa akiwa ni rehma kwa ulimwengu wote na ni dalili za wazi kwa waja wake wote.na ziwe juu ya watu wake na maswahaba zake ambao walio beba kitabu cha mola wao Mtukufu, na Sunnah za Mtume wao Rehma na amani za Allah ziwe juu yake -kwa wale watakao kuja baada yao, kwa uaminifu wa hali ya juu na umakinifu na kwa kuhifadhi kuliko kamilika kwa maana zake na matamshi yake- Allah aliwaridhia na akawafanya watu wawaridhie na Allah atujalie katika wafuasi wao kwa wema.